Sunday, 9 August 2015

Edward Lowassa kuchukua fomu ya uraisi kesho Jumatatu 10/08/2015

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kesho atachukua fomu za kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati msafara wake utakapoanzia ofisi za makao makuu ya CUF kuelekea ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na baadaye kwenda kumalizia makao makuu ya Chadema yaliyoko Kinondoni.

Safari ya Lowassa, ambaye anawania urais kwa tiketi ya Chadema na chini ya mwamvuli wa vyama vinne vya CUF, NCCR-Mageuzi, Chadema na NLD, itakuwa ya umbali wa kilomita 11, ikihusisha wilaya mbili za Ilala na Kinondoni.

“Yeyote anayejisikia kutaka kumsindikiza Lowassa, anakaribishwa,” alisema kaimu katibu mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu jana alipozungumza na waandishi wa habari.




0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2014 KaribuVijana